Kwa mujibu wa kitengo cha kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, Katibu Mkuu wa Kata’ib Sayyid al-Shuhada (Muqawama wa Kiislamu wa Iraq), kupitia ujumbe alioutoa na kuchapishwa katika mtandao wa X, alisisitiza kwamba: Kupambana na vitisho dhidi ya dini na taifa ni ahadi thabiti na wajibu mtakatifu ambao hatutauacha kamwe.
Tarjama ya ujumbe wake ni kama ifuatavyo:
“Sisi ndani ya Kata’ib Sayyid al-Shuhada tunaamini kwamba; muqawama ni wajibu kama agano ambao hauwezi kuepukwa, na ni wajibu kama swala ambao hauwezi kupuuzwa. Na yeyote anayefikiri kwamba tutavunja agano letu au tutaacha swala, basi abebe pia dhana hiyo [batili] kwamba inawezekana tuache muqawama.”
Maoni yako